NIMEMUONA YEYE AMBAYE AMENIONA.
NIMEMUONA
YEYE AMBAYE AMENIONA.
Tamani
kumuona yeye anaekujua wewe tangu siku ya kwanza ya kuumbwa kwako siyo
mwanadamu ambae hajui hatma yako, Lipo jambo ambalo unalitaabikia mtafute Yule
anaekuona ili akupe haja yako (2Wafalme 19:27-28).
Usiitumie vibaya neema ya Mungu kwa kufanya
dhambi kwa makusudi na kutegemea kwamba utaingia magotini na kuomba rehema Mungu
hajaribiwi na unapoamua kumtafuta yeye anaekuona maanisha kumtafuta nae
atajidhirihisha kwako usitumie njia ya mkato ili kukidhi hitaji lako kwa maana
itakugharimu.
Mtafute yeye
naekuona Mungu wetu ni Mungu mwaminifu hakumuumba mwanadamu ili apate taabu, apate
shida ila alimuumba kwa kusudi maalum na lazima litimie kwako, Kaa utafakari ni
kwa nini unapitia hali uliyonayo sasa usianze kulaumu, na kudhani kwamba Mungu
hakuoni, Tamani kumuona yeye anaekuona ili akuvushe kwenye daraja unalopitia
usimtazame mwanadamu mtazame Mungu anasema nini juu ya maisha yako.




Maoni
Chapisha Maoni